Wednesday 19 December 2012

Morogoro all stars - Karibu Morogoro

Afande Sele

Intro
Na na na na na na na naa na na na na naaa M-O-R-OOoh,
moro town yeah! Home sweet home x2 (uuh)

Ubeti wa kwanza - Stamina

Chunga usipitilize stendi suka acha watu msamvu,
Moro imenipa mengi, washkaji pesa na shavu,
hatuna mpango na bahari, Mbona hata mindu ina fukwe,
Milima kwetu fahari, mwaka mzima kwetu full kipupwe,
Ausindile anoga ndio swagga za waluguru,
hata ufunge kwa kuroga ila Moro itaniacha huru,
sihitaji tena Baga utamu naupata Gairo,
Masai wote huu wana swagga karibu kama upo Njiro,
Toka enzi za Mbaraka mpaka wajukuu wa Mwinshehe,
Mkude kusimama Pastor, Mbokeleni kuwa sheikh,
Nina haki ya kujisifu, moro imenipa kitalu,
Namwaga Pombe kwa chifu wa Moro babu Kingaru,
Sina bifu na Mngoni, Mpogoro ndio napodeka,
Anzisha tifu ulingoni usande tukupe Cheka,
Mliotutoka kimwili Kiroho tupo pamoja,
Karibu Moro mswahili uzalendo uende kwa hoja,
(uuuuuh hu huuu)

Kiitikio

Karibu Morogoro, watu wote wa bara, visiwani mpaka Zanzibar,
Bahari sio kasoro, wageni karibuni hapa kwetu mtapata furaha, x2
Urithi burudani vyote shwariiiiii, karibu mji kasoro,
Udzungwa ujionee ehee hee hee hee hee heee he mwenyewe,
Usisubiri usimuliweee, mwenyeweee (Yoo) Njooow

Ubeti  wa pili – O - ten

Yeah! mji unaweza poa, niko rock juu mlimani,
Na mimi ndio mkuu wa mkoa karibuni madizini,
Matonya alifukuzwa Dar breki ya kwanza akaja shaini,
Mandela alikuwa shujaa, moro akaifanya maskani,
Si unajua? Miji kibao haipati mvua,
tofauti kubwa hapa kwetu inanyesha mpaka inaua,
Mzinga,  Ndigutu, Kichangani, Kiguru nyembe, hapa kwetu haina uzembe,
Hata star anashika jembe, Natokea matombo kilosa narudi mzumbe,
Nampitia Mkude, makala yuko wapi Msinde,
Moro Bambam ila vichwa visivimbe, narudi shamba hata muziki nisiimbe,
No, mi na moro tupo kama pacha, yes karibu moro tuishi kama kacha,
Mbuga zipo na hata madini yapo, palipo na amani ndo mi nilipo

Kiitikio

Ubeti wa tatu- Afande Sele
Morogoro,mjini kwetu,
Karibuni wote rafiki na ndugu zetu(shua)
Toka pande zote iwe ndani, mpaka nje ya nchi yetu,
Karibuni kwetu mtembeee, harakati zetu mjionee,
Kama mimi na mtu chee, kuna mashamba tunalimaga,
Mboga mboga na mipunga, kuna mahindi, kuna matunda, viazi miwa na karanga,
Karibuni nyote Morogoro mchote, hekima za Selemani mtangaze mataifa yote,
Mkawaambie, mlichokiona hapa, mkawasimulie siri ya cheka kuwa chapa,
Na habari kibao za wakali wa hapahapa, kwa soka kwa hip hop, ma streika marapa,
Maboxer, madensa wote waliotoka hapa, wahapahapa, tangu kitambo kile,
Kabla ya Afande Sele, Kabla ya O ten na Belle, kabla ya Supa Ngedere Moro Bado Chapa Ilale
Ngoma inogile, tuna historia tele,
 hata mawlimu Nyerere alikuwaga Mbunge wa Kwanza wa Moro miaka ile,
kwa wasiotambua hilo. Karibuni Moro, hata tommorow
karibuni mjionee maajabu ya mzimu wa Kolelo, ifakara Kilombero,
Tuliani, Mvomero, Kilosa na Msowero, Masombo mpaka Gairo
Yeaaah hii ndio Morogoro mpaka Nyachiro kwa mjomba Kobelo
Na Mahenge kwa shangazi wa kipogoro, twende mahewaa

Kiitikio

Kibwagizo

Morogoro mji kasoro bahari kwetu bado shwari
Morogoro, Mgeta Mzumbe Mlali Moro imetulea
Nilipokula gimbi na kachumbari, mwenzenu mimi naona fahari
Hata ninapokwenda mbali nitarudi moro nyumbani
Nimelelewa angali bado kichanga, bado mimi sijajua kuimba
Mpaka sasa mimi natamba, tena Moro nimepata Mchumba mie x2
Nitazikwa Moro, Nitakufa Moro, Naipenda Moro, nitaishi Moro

Kiitikio




No comments:

Post a Comment