Monday 31 December 2012

Mtoto amekua - Pasha ft Tunda


Pasha na Tundaman

Intro -Tunda

Ahaaaaaa ayeye yeeee huuuuuuu

Pasha

Waswahili husema mtoto umleavyo ndivyo akuavyo-oo,
Staki kuamini huu usemi bora niache tu mambo kama yalivyo-oo,

Tunda

Shemeji  nivipi hasa, kisa mkasa mpaka unalalamika hivyo-o,
Nini kimekupata, naona ka’ umedata sijakuzoea hivyo-o,

Pasha
Naona kwangu hili ni balaa,  binti anashinda tu baa,
Anakata kata tu mitaa, huyu binti kiruka njia,

Tunda
Elewa Yule mtoto washule, baa anatafuta visoda vya kufanyia tu hesabu-u
Shemu hemu punguza ghadhabu, yeye ndo anazurura vipi anakuadhibu-u?

Pasha
Ananifanya nakosa amani, wananicheka majirani,
Kila nakopitapita mtaani vidole nanyooshewa mimi,
Ona mama yake nilipomuoa, alikuwa na maadili mema,
Hata baba yake  nimelelewa kwenye familia njema,

Tunda
Mtoto wa nyoka ni nyoka, mi bado sijachoka atamfuta tu mama yake,
Huyu ado hajadondoka, bado hajapotoka, atamfuata tu mama yake,

Kiitikio  x2
Pasha
Wee shemeji yangu,(shemeji yangu) bado tu hujajua,
Mbona mi nshatambua, binti ameshakua, ha haaa

Tunda
Shemeji yangu mtoto dunia inamzuzua, utoto unamsumbua,
Nakuahidi ataacha akikua,

Ubeti 2
Pasha x2
Wiki nzima ndani hajalala, kutwa anashinda kuzurura,
Hata sijui anachokula, Mola atamlinda inshaalah,

Tunda
Wiki jana ye aliniga kwamba anakwenda shule kujisomea,
Labda unalingine kwa hilo jambo mi namtetea,
Ni kweli aliniaga samahani shemu mi sijakwambia,
Naomba unambie kingine ila kwa hilo unamsingizia,

Pasha x2
Hizo nguo zake ndizo zinazo nichanganya mwenzenuuu,
Sina raha akipita nilipokaa,
Hajali lolote hata kama hiyo siku wamekuja wageniii,
Apotezea, she don’t care natamani kuliaaa,

Kiitikio  x2
Pasha
Wee shemeji yangu,(shemeji yangu) bado tu hujajua,
Mbona mi nshatambua, binti ameshakua, ha haaa

Tunda
Shemeji yangu mtoto dunia inamzuzua, utoto unamsumbua
Nakuahidi ataacha akikua

Kibwagizo
Pasha
Mtoto ameharibikaa x2
Mtoto ameharibika, ameharibika, ameharibikaa

Tunda
Mtoto hajaharibika, hajaharibiuka, hajaharibika x2

Pasha
Ona ameharibika x 2
Ona ameharibika, ameharibika, ameharibikaa

Outro
Tunda
Huuuuuuu, yiiiiiiiiii mmmh x3
Shebi fleva mwana, Shebi fleva mwanangu, Shebi piga vinanda mjomba anaonewa sana
Shebi piga vinanda, Shebi fleva piga vinanda, Shebi piga vinanda mjomba wangu anaonewa sana
Mmmmh! Mh mh mh Shei fleva kiboko yao









No comments:

Post a Comment